Kivuko Na Watoto: Mafunzo yenye kuleta mabadiliko kwa watoto na walezi wao waliioathirika na VVU
472Kivuko Na Watoto: Mafunzo yenye kuleta mabadiliko kwa watoto na walezi wao waliioathirika na VVU
472Paperback
-
PICK UP IN STORECheck Availability at Nearby Stores
Available within 2 business hours
Related collections and offers
Overview
Product Details
ISBN-13: | 9781853399138 |
---|---|
Publisher: | Practical Action Publishing |
Publication date: | 07/31/2016 |
Pages: | 472 |
Product dimensions: | 6.25(w) x 9.75(h) x (d) |
About the Author
Gill Gordon
What People are Saying About This
UKIMWI unahusu haki ya kijamii. Hatuwezi kufikia malengo yetu ya kutokomeza UKIMWI ifikapo mwaka 2030 mpaka tutimize mahitaji ya jamii nyingi zinazoishi katika mazingira magumu, mara nyingi watoto na vijana wanaoishi na VVU na wanaoathiriwa na virusi. Kivuko na Watoto inatoa njia ambayo jamii zinaweza kusaidia na kulea watoto hawa na kujenga uthabiti wao. Hili ndilo ambalo ni lazima tulifanye kwanza – kuwajali wanaoishi katika mazingira magumu. Michel Sidibe, Mkurugenzi Mtendaji wa UNAIDS ‘Huu ni mwongozo muhimu sana kwa watoto na walezi. Mwongozo huu utasaidia kujenga uhusiano wa karibu zaidi kwa kutumia mawasiliano yenye maana/muhimu yanayosaidia watoto na walezi kukabili vikwazo na kujenga kaya iliyofungamana na kusaidiana.’ Martha Tholanah, Mwenyekiti wa Kimataifa, International Community of Women Living with HIV/AIDS ‘Natamani kuwa watoto wote wenye umri wa miaka 5 – 14 na walezi wao walioathiriwa na VVU wangepata fursa ya kufurahia Kuvuko na Watoto. Ninaamini kwamba kitawasaidia kutimiza ndoto zao na kushinda changamoto zao. Ni mwongozo wa kipekee kwa sababu unashughulika na makundirika peke yao na kwa pamoja na kushughulikia masuala mengi – ya kisaikolojia, kimwili, kijinsia, kiyakinifu na kiroho – yenye umuhimu mkubwa kwetu sisi sote’ Vincent Mwale, Waziri wa Vijana na Watoto, Zambia ‘Programu na miongozo kama Kivuko na Watoto vinaweza kuleta mabadiliko makubwa kwa binadamu kati ya maendeleo bora na dira ya dunia yenye uwezekano, na katika matukio ya upeo wa juu, maisha yaliyozingirwa na kifo.’ L'Orangelis Thomas, mwanamke kijana anayeishi na VVU ‘Gill Gordon hana budi kupongezwa kwa kuandika mwongozo unaovutia kusoma na kutumika. Kivuko na Watoto kimejaa vidokezo halisi vya namna ya kutenda, na muhimu zaidi kina hazina/mkusanyiko wa kutosha wa mazoezi kwa vitendo. Kitabu hiki kitakuwa marejeo yanayofaa zaidi kwa daktari yeyote anayewashughulikia watoto wanaoishi katika mazingira magumu na vijana.’ Morten Skovdal, Profesa Mshiriki, Department of Public Health, Universityof Copenhagen ‘Inafurahisha sana kuona upeo wa fikra muhimu na vitendo katika kushughulikia watoto walioathiriwa na VVU. Marejeo haya yanatoa programu bora ya mafunzo inayotokana na mafanikio makubwa ya Kivuko na Watoto. Iwapo tutakipa muda wa kutosha na nia thabiti kwa mbinu yake ya kufundishia, Kivuko na Watoto kina uwezo mkubwa wa kushughulikia upungufu muhimu katika mwitikio wetu kwa watoto walioathiriwa na VVU .’ Kate Iorpenda, Mshauri Mwandamizi, Watoto na Vijana Balehe, International HIV/AIDS Alliance ‘Mwanzoni wakati PASADA ilipoanza kutumia Kivuko, watu walidhani shirika hilo lina wazimu. Baadaye walitambua kuwa kilikuwa ni nyenzo muhimu na yenye uwezo mkubwa kwa jamii. Laiti sauti yangu ingeweza kusikika duniani kote ningewaambia watu watumie Kivuko na Watoto kwa sababu kitabadili maisha yao na namna wanavyojifikiria kuhusu VVU na UKIMWI.’ Mrisho Mpoto, Mshairi, Mwigizaji na Mwanamuziki ‘Gill Gordon ana kipaji kikubwa cha kuandika miongozo inayochochea kujitambua na wakati huo huo kujenga kujiamini, kuthubutu, na stadi nyingi muhimu za maisha. Analeta utajiri wake mkubwa wa uzoefu wa kufanyakazi pamoja na vijana katika masuala mengi tofauti. Bila ya shaka, nitayatumia mawazo haya na kuyatohoa kwa ajili ya watoto wadogo katika miktadha mingine.’ Ross Kidd, Participatory Mkufunzi Shirikishi na Mwandishi wa miongozo mbalimbali, ikiwemo Kuelewa na Kukabili VVU ‘Tunapenddekeza kwa dhati, Kivuko na Watoto kuwa kitabu pekee katika kusaidia utekelezaji wa ujinsia na afya afya ya uzazi na VVU na UKIMWI kwa Watoto.’ Zikhalo Phiri, Mtendaji Mkuu wa Young, Happy, Healthy and Safe, Zambia